RAINFORD KALABA ARUHUSIWA KUTOKA HOSPITALI





Kiungo wa zamani wa klabu ya TP Mazembe, Rainford Kalaba ameruhusiwa kutoka hospitalini baada ya kujeruhiwa vibaya katika ajali ya gari iliyotokea mwanzoni mwa mwezi huu.

Nahodha huyo wa zamani wa Chipolopolo alikuwa akiendeshwa katika gari aina ya Mercedes-Benz iliyogongana uso kwa uso na lori katika tukio la kutatanisha ambalo awali ilihofiwa amepoteza maisha yake.

“Rainford Kalaba ameruhusiwa kutoka UTH-Adult ambapo alilazwa baada ya kuhusika katika ajali ya barabarani wiki mbili zilizopita,” alisema Ofisa wa Hospitali ya Mafunzo ya Chuo Kikuu, Nzeba Chanda katika taarifa iliyotolewa.

“Leo (Ijumaa Aprili 26) inaadhimisha siku 14 kamili tangu wakati wa kulazwa kwake. Ataenda kuendelea kuuguzwa katika nyumba ya familia yake.”

Wanasoka mbalimbali wameonyesha kumuunga mkono Kalaba, wakikumbuka mchango wake katika soka la Zambia kama kiungo mahiri na kiongozi.


 

0 Comments

Post a Comment

Post a Comment (0)

Previous Post Next Post