"Tunamshukuru kuna makundi yametoka Temeke bila kujali siasa, kuna watu kule Temeke walikuwa wanapiga maneno ya siasa, maana wale bio zimewashinda sasa wanapiga maneno mengi, ukiona mtu ana maneno maneno zaidi na umwoni barabarani kukimbia ameshashindwa.
Huu mchezo wetu (Jogging) ni mchezo wa wazi sasa wewe barabarani atukuoni kazi kuandika maneno tu waraka mrefu" alisema Kitenge, Muasisi wa Wasafi Jogging Club.
VIDEO HII HAPA CHINI
Utakumbuka Januari 12, 2025, Chama cha Jogging wilaya ya Temeke (TEJA) kilipiga marufuku vilabu vya Jogging katika wilaya hiyo kushiriki katika Bonanza la Wasafi Jogging kutokana na sababu nyingi walizo zitoa TEJA katika taarifa yao.
Na moja ya sasabu walizotaja TEJA kuzuia vilabu vya Temeke kushiriki Bonanza hilo ni kulinda hadhi ya chama na wanachama wake (Vilabu) kwa kutumiwa ama kudharauliwa na kutolewa kejeli na baadhi ya viongozi wa Wasafi Jogging Club.
PICHA ZA MATUKIO YA BONANZA LA WASAFI JOGGING CLUB









.jpg)







Post a Comment